Jumamosi, 26 Aprili 2014 05:20

Je bado unatumia Joomla 1.5? Ni muda wa kusasisha (upgrade) sasa!

Written by
Rate this item
(0 votes)

Katika makala zangu zilizopita, nimeongelea umuhimu wa kusasisha (asante Kaka Hassan kwa kuniongezea msamiati mwingine), sio tu utaongeza ufanisi na usalama wa wavuti yako, bali pia itakuwezesha kuhakikisha unakuwa na wavuti salama na iliyo bora. Ingawa mengi yameiongelewa, mengi yameandikwa, lakini ni ukweli usiopingika kuwa wengi wetu bado tunatumia Joomla 1.5.

Sababu kubwa inawezekana ni kutokana na hofu ya kuhamia Joomla 2.5 kwani kuhama toka Joomla 1.5 kwenda 2.5 ni kama kuhamisha wavuti nzima hivyo wamiliki wengi wa wavuti wameona bora nusu shari kuliko shari kamili hivyo wameamua kubaki kwenye Joomla 1.5, ila mimi nasikitika kukutaarifu kuwa hiyo ni dharuba, bora masika kuliko Tsunami.

Kwakuwa hakuna tena masasisho kwenye Joomla 1.5 , hivyo basi inakabiliwa na vihatarisho lukuki. Kwa lugha nyingine tunaweza kusema, upo kwenye hatari.

Ili kuwasaidia wamiliki ambao bado wanafikiria ama waende Joomla 2.5 ama wabaki kwenye Joomla 1.5, fuatilia mchoro wa chini.

Pia unaweza kuishusha picha hii kwa kwenda Hapa.

Hassan Ayeko

Hassan ni mtaalamu wa masuala ya IT pia ni mkalimani mkuu wa Joomla Kiswahili (Joomla Coordinator for Swahili language)

www.att-center.de